We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, June 27, 2019

RITA kutoa vyeti vya kuzaliwa Maonesho Sabasaba

Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA), utatoa elimu na huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi hiyo ikiwamo vyeti vya kuzaliwa katika Maonyesho ya biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yatakayoanza kesho katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam.
Meneja Masoko na Mawasiliano wa RITA, Josephat Kimaro amesema mbali na kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa pia wakala utatoa ushauri wa kisheria bure kuhusu masuala ya kuandika wosia na mirathi.
“Pia tutapokea maoni, maswali, ushauri na mapendekezo kuhusu huduma za Wakala,” amesema.
Kimaro amesema RITA imekuwa ikishiriki maonesho hayo kila mwaka ambapo mwaka jana RITA ilishiriki na kutoa huduma kwa zaidi ya wananchi 5,524 ambao walisajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list