Leo Alhamisi jioni Yanga itakuwa dimba la Uhuru kuikabili Tanzania Prisons katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara
Yanga itamkosa mlinda lango Klaus Kindoki anayetumikia adhabu ya kadi tatu za njano
Pia beki wa kushoto Gadiel Michael alipata majeraha katika mchezo uliopita dhidi ya Azam Fc anatarajiwa kukosekana pamoja na mkongwe Kelvin Yondani ambaye leo anamaliza adhabu ya kukosa michezo mitatu
Yondani atarejea kikosini kwenye mchezo wa nusu fainali kombe la FA (ASFC) dhidi ya Lipuli Fc utakaopigwa mkoani Iringa, May 06 uwanja wa Samora
No comments:
Post a Comment