Kiongozi mkuu wa Kanisa katoliki duniani, Papa Francis amewaonya mashabiki wa mshambuliaji wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi kwa kuwataka waache kumfananisha mshambuliaji huyo na ‘Mungu’ .

Papa Francis akihojiwa kwenye kituo cha runinga cha Spanish TV, aliulizwa na mtangazi wa kituo hicho, Jordi Evole kwenye kipindi cha ‘Salvados’ kuwa “Kuna baadhi ya watu wanamuita Lionel Messi Mungu wa mpira duniani, je wewe unaweza kumuitwa Mungu“.
“Papa Francis alijibu “Kumfananisha Mungu na Messi sio sawa kabisa, nadhani mashabiki wanatakiwa kujua namna ya kutumia vizuri jina la Mungu.” amesema Papa Francis na kufunguka zaidi.
“Watu wengi wanamtaja Mungu kama wanavyotamka ‘Nakupenda sana’, jambo hilo limesababisha hadi waone jambo la kawaida kusema ‘Messi ni Mungu wa mpira’ lakini huo ni utovu wa nidhamu na haikubaliki,“amesema Papa.
Lionel Messi na Papa Francis wote ni raia wa nchi moja Argentina, na kipindi cha nyuma Papa Francis aliwahikumpongeza Messi kwa kuwashawishi vijana wengi kupenda mpira wa miguu.
No comments:
Post a Comment