We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, April 1, 2019

CCM yataka ufuatiliaji makini na ushirikishaji wananchi miradi ya maendeleo



Na Ahmad Mmow, Nachingwea.

Chama Cha Mapinduzi(CCM), mkoa wa Lindi kimeziomba  taasisi za serikali zenye dhamana ya kufatilia ubora na matumizi ya  fedha zinazotumika katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani humu.

Wito huo ulitolewa jana na mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Lindi, Fadhily Mohamed kwenye kongamano la maadili lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa shule ya sekondari Nachingwea, iliyopo mjini Nachingwea.

Mohamed alisema kunaumuhimu mkubwa wa taasisi hizo kufuatilia matumizi ya fedha na ubora wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa mkoani humu ili kuepuka hasara zinazosababishwa na ufisadi unaofanywa na baadhi ya watumishi wasio waadilifu.

Alisema nijambo la kusikitisha kuona baadhi ya miradi ya maendeleo imekwama au kutumia fedha nyingi kuliko ukubwa wa miradi inayotekelezwa.Hali ambayo inachangia kukwamisha mipango ya serikali ya kuwahudumia na kuwapelekea maendeleo wananchi.

"Mfano ni fedha zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya cha Kilimarondo zinalingana na zilizotolewa kwa ujenzi wa kituo cha afya cha Mpengere. Lakini Mpengere kimefikia hatua mzuri, tofauti na Kilimarondo," alisema Mohamed.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list