We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, March 25, 2019

Zitto Kabwe azungumzia nguo ya Rais Magufuli

Zitto Kabwe azungumzia nguo ya Rais Magufuli
Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amefunguka kuwa ushindi wa Taifa stars jana dhidi ya timu ya taifa ya Uganda 'The Cranes' umeliunganisha taifa pasi na kujali itikadi za vyama.

Zitto kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika kuwa, ''mpira umeleta muunganiko kwa taifa na kuleta furaha nchini, huku akifurahishwa na shati alilokuwa amevaa Rais Magufuli lenye rangi ya zambarau ambayo ni rangi  inayotumiwa na chama chake.

"Nguvu ya mpira kuunganisha nchi ni ya aina yake. Kina Samatta kuwezesha Tanzania kufuzu ‘Mataifa Huru Afrika’ #AFCON nchi iliyokuwa imenuna, imejawa furaha. Hata Rais kuonyesha Umoja alivaa shati la Zambarau, rangi ya Chama Cha ACT-Wazalendo akitazama mechi Ikulu", ameandika Zitto.

Taifa Stars imeungana na timu ya taifa ya Uganda, Kenya na Burundi zitakazoiwakilisha Afrika Mashariki katika michuano ya AFCON itakayofanyika kuanzia mwezi June hadi Julai, 2019 nchini Misri. 

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list