We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, March 28, 2019

Zahera ataja sababu ya kumuacha Ajib Dar


Nahodha wa kikosi cha Yanga Ibrahim Ajib hajasafiri na timu hiyo kuelekea mkoani Mwanza ambapo keshokutwa Jumamosi itashuka katika uwanja wa CCM Kirumba kuikabili Alliance Fc kwenye mchezo wa robo fainali, kombe la FA


Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema Ajib hakujumuishwa katika kikosi kwa kuwa bado hajawa 'fit' tangu apone majeraha ya misuli
Zahera amesema Ajib anahitaji muda zaidi wa kufanya mazoezi ili aweze kuwa tayari kurejea dimbani
Akizungumzia mchezo huo, Zahera amesema wamejiandaa kikamilifu kuikabili Alliance Fc ambayo inaonekana kupania zaidi mchezo huo

"Tunaufahamu ubora wa Alliance Fc na hata udhaifu wao pia tunaujua, hatuna wasiwasi kuelekea mchezo huo," amesema Zahera

Mcongoman huyo aliyerejea usiku wa kuamkia jana na kuungana moja kwa moja na kikosi cha Yanga, amesema atatumia siku ya leo na kesho kufanya maandalizi ya mwisho tayari kwa mchezo huo utakaopigwa Jumamosi March 30 katika dimba la CCM Kirumba

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list