We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, March 28, 2019

Mahakama yaitaka serikali kurekebisha sheria ya vyombo vya habari


Mahakama ya jumuiya ya Afrika Mashariki imetoa hukumu ya kesi ya kupinga ukandamizaji wa uhuru wa vyombo vya habari chini iliyokuwa imewasilishwa na Baraza la habari Tanzania (MCT) na kituo  cha sheria na a haki za binadamu pamoja na Mtandao wa utetezi wa haki za binadamu. 

Katika hukumu hiyo ya kesi namba 2 ya mwaka 2017 iliyosomwa na Jaji wa mahakama hiyo Charles Nyachae mahakama hiyo imeitaka serikali ya Tanzania kurekebisha baadhi ya vifungu vya sheria kwani vimeonekana kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari 

Akizungumza baada ya hukumu hiyo kutolewa Katibu Mtendaji wa Baraza la habari Tanzania Bw Kajubi Mukajanga amesema haki imetendeka na ameendelea kuwataka wadau wa vyombo vya habari wakiwemo waandishi , wahariri kuendelea kutekeleza wajibu  wao na akasisitiza umhimu wa kufuata sheria. Mwaka 2016 Bunge lilipitisha sheria ya huduma za habari,sheria ambayo wadau wa habari na wanaharakati waliilalamikia na kuipinga kwa kile kilichodaiwa kukandamiza uhuru wa habari.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list