We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, March 27, 2019

Video: Ridhiwani Kikwete akabidhi mradi wa maji safi na salama

Mbunge wa Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ridhiwan Kikwete amekabidhi mradi wa maji safi na salama katika shule ya Sekondari Mboga iliyopo Jimboni humo.
Akikabidhi kisima hicho, Kikwete amewataka walimu na wanafunzi kutumia kisima hicho kwa uangalifu wa hali ya juu ili kiweze kudumu kwa muda mrefu zaidi.
Pia Ridhiwani amewataka walimu kuwaruhusu wananchi wanaozunguka maeneo hayo kutumia maji hayo ili na wao wanufaike kupitia kisima hicho ambacho kimekuwa ni mkombozi kwa shule na wananchi.
Aidha, sambamba na kukabidhi mradi huo wa maji, pia amezindua mabweni ya wasichana katika shule hiyo na kuahidi kuendelea kujenga mabweni mengine ya wavulana ambapo amesema mabweni hayo yataweza kuwapunguzia adha mbalimbali wanazo kumbana nazo wanafunzi hao.
”Tukishamaliza kujenga mabweni ya wavulana, mahitaji ya maji yatakuwa makubwa zaidi, hivyo sisi viongozi tutajenga tanki kubwa lenye ujazo mkubwa zaidi ili kuweza kuendana na mahitaji yatakayokuwa yanahitajika kwa kipindi hicho,”amesema Kikwete



No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list