We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, March 28, 2019

Tetesi za soka barani Ulaya Alhamisi hii, Hudson-Odoi, Sanchez, Rashford, Maguire, Chilwell

Barcelona wapo tayari kuwapa Manchester United kiungo Philippe Coutinho, 26, ama Malcom, 22, kama sehemu ya ofa ya kumnasa mshambuliaji Marcus Rashford, 21. (Mundo Deportivo, via Mail)



Klabu ya Borussia Dortmund inasisitiza kuwa haina mpango wa kumuuza mchezaji wao raia wa Uingereza Jadon Sancho, 19, ambaye amekuwa akihusishwa na Manchester United. (Mirror)
Chelsea wanaweza wakasikiliza ofa za usajili za zaidi ya Pauni milioni 43 ili kumuachia mshambuliaji kinda wa Uingereza Callum Hudson-Odoi, 18. (Sport Bild, via Metro)
Leicester hawapo tayari kuwatoa mabeki wake Harry Maguire, 26, na Ben Chilwell, 22, ambao wamekuwa wakinyemelewa na vilabu vikubwa vya Manchester United na Manchester City. (Mirror)
Manchester United hawana mpango wa kumuuza mchezaji wao anayepokea mshahara mkubwa zaidi, Alexis Sanchez, 30, licha ya kutoonesha makali uwanjani na ripoti kuwa suala la mshahara wake linatatiza mapatano ya mkataba mpya na kipa David De Gea. (London Evening Standard)
Beki wa Liverpool Dejan Lovren ananyemelewa na vilabu vikongwe vya Italia, Roma, Napoli na AC Milan ili wamsajili mwishoni mwa msimu. (Mirror)
Manchester City ni miongoni mwa vilabu ambavyo vinamfuatilia kwa karibu winga wa Swansea na Wales Dan James, 21. (Sun)
Mshambuliaji kinara wa klabu ya Tottenham Harry Kane, 25, amesema anataka kucheza kwenye ligi ya Marekani NFL “ndani ya miaka 10 au 12 ijayo”. (ESPN)
Kiungo wa Liverpool na Serbia Marko Grujic, 22, ambaye yupo kwa mkopo katika klabu ya Hertha Berlin, anataka kusalia kwenye klabu hiyo ya Ujerumani walau kwa mwaka mmoja zaidi. (Liverpool Echo)
Mshambualiaji wa raia wa Paraguay Sergio Diaz, 21, atasalia Real Madrid baada ya klabu ya Corinthians ya Brazil, ambako amekuwa kwa mkopo msimu huu kuamua kuwa hawatamnunua. (Marca)

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list