We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, March 26, 2019

Sakata la uwanja wa Taifa kujaa juzi, Waziri Mwakyembe aomba radhi


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amewaomba radhi Watanzania wote waliojitokeza kwa wingi Uwanja wa Taifa juzi kushuhudia mechi ya kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika, Afcon 2019 na kushindwa kuingia kutokana na uwanja kujaa.

Stars, juzi iliifunga Uganda mabao 3-0 na kufuzu fainali za Afcon zilizopangwa kufanyika Misri Juni mwaka huu.

Tanzania imefuzu kwa mara ya kwanza baada ya miaka 39. Katika mechi hiyo iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, mashabiki walikuwa wengi na kujaa uwanjani mpaka ikatangazwa milango ifungwe wasiingie tena hivyo wengi walibaki nje na wakati mwingine polisi walilazimika kuwatawanya na mabomu ya machozi.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Lindi, Mwakyembe amesema wizara yake inaichukua changamoto hiyo kama funzo na katika mechi za Kimataifa zijazo itahakikisha inaweka runinga kubwa na nyingi kwenye viwanja vingine ili watakaokosa nafasi ya kuingia nao waone mechi husika.

"Mimi kwa sababu naiongoza wizara ya habari na michezo, niwaombe radhi watanzania waliomiminika uwanja wa taifa wakakosa nafasi," alisema Waziri Mwakyembe.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list