We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, March 27, 2019

Mabosi wa Simba wamnunulia ndinga Aussems


Mabosi wa timu ya Simba SC wamemnunulia gari mpya Kocha Mbelgiji, Patrick Aussems katika kuhakikisha kikosi cha Simba kinafanya vizuri kwa kuwekwa hamasa ya nguvu. 

Gari hilo ambalo ni aina ya Toyota Wish, Aussems ameanza kulitumia jana wakati kikosi cha Simba kikijifua kwenye Uwanja wa Bocco Veterani kwa ajili ya mechi zijazo za ligi. 

Awali Kocha huyo alikuwa akitumia gari ambayo ilikuwa inatumiwa na Makocha waliopita akiwemo Joseph Omog, Jackson Mayanja na Pierre Lechantre. 

Taarifa zinasema Aussems aliomba kubadilishiwa ndiga hiyo ili aweze kutimiza majukumu yake ya kazi vizuri na kwa ufasaha zaidi. 

Wakati huo kikosi cha Simba kinaendelea kujiandaa na mechi ya ligi ambapo wikiendi ijayo kitakuwa na mchezo dhidi ya Mbao FC, mechi ikipigwa Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro. 



No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list