We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Friday, March 29, 2019

Kwanini muagize nguzo nje ya nchi? - Naibu Waziri Nishati awahoji Wakandarasi


Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amewaonya wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini kuzingatia masharti yaliyowekwa na serikali hususani kutumia vifaa vya ndani ya nchi, na kwamba atakayeona hawezi kutekeleza masharti hayo, arudishe kazi hiyo kwa Serikali ili apewe mkandarasi mwingine.

Alitoa onyo hilo jana, Machi 28, 2019 katika kijiji cha Ngazi, wilayani Lushoto, Mkoa wa Tanga, wakati akizungumza na wananchi, kabla ya kuwasha rasmi umeme katika kijiji hicho.

“Kwanini muagize vifaa kama nguzo nje ya nchi wakati sisi bado miti tunayo na mingine imepandwa kwa makusudio hayo?”

Alisisitiza kwamba wakandarasi wanaochelewesha kazi kwa visingizio vya namna hiyo waache mara moja kwani sababu hizo hazina mashiko.

Naibu Waziri alilazimika kutoa onyo hilo kufuatia kazi duni ya mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Umeme Vijijini, Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Kwanza (REA III – I) wilayani Lushoto, ambao ni muunganiko wa kampuni za Njarita, Aguila na Radi.

Alipohojiwa kuhusu suala hilo, Mkandarasi husika alitoa utetezi kwamba mojawapo ya sababu zilizofanya acheleweshe kazi ni agizo la serikali linalowataka wakandarasi kutoagiza vifaa nje ya nchi, badala yake watumie vifaa vya ndani ya nchi.

Akijibu utetezi wa mkandarasi husika, Naibu Waziri alimtaka kujitathmini kuona kama anakidhi vigezo kwani wenzake wanaotekeleza miradi ya aina hiyo sehemu mbalimbali za nchi wanafanya vizuri.

“Tumewasha vijiji zaidi ya 1,900 katika Mradi wa REA III na karibu kila Mkoa na Wilaya, vijiji vimewashwa. Wewe uliomba kazi hii na unashindwa. Inakuwaje wenzako wanaweza?

Akifafanua zaidi, Naibu Waziri alisema kuwa kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali ya Awamu ya Tano, inayoongozwa na Rais John Magufuli, matarajio ni kuwa, ifikapo Juni 2021, vijiji vyote vilivyokuwa havina umeme tangu serikali husika iingie madarakani, ambavyo vilikuwa takribani 7,873; viwe vimepata umeme.

Alisema, wakati mwingine baadhi ya wakandarasi wanarudisha nyuma jitihada hizo ndiyo maana Serikali ikaunda kamati mbalimbali za usimamizi. Aliwataja wasimamizi wa miradi ya REA kuwa wanatoka ngazi ya Wizara, REA, Meneja Tathmini wa Mkoa, mafundi mchundo wa Wilaya pamoja na wasimamizi wa Kanda.

“Hata hivyo, mwisho wa siku, msimamizi mkuu ni Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya wakishirikiana na Kamati za Ulinzi na Usalama za maeneo yao,” alibainisha.

Katika hatua nyingine, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Ngazi wilayani Lushoto, kabla ya kuwasha rasmi umeme katika kijiji hicho, Naibu Waziri alisisitiza kuwa gharama ya kuunganishiwa umeme kwa wananchi wa vijijini ni shilingi 27,000 tu.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list