We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, March 28, 2019

Hii ndio Super Sports FC aliyokwenda kufanya majaribio Gadiel Michael wa Yanga

Beki wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars na club ya Yanga SC Gadiel Michael Mbaga ameondoka nchini leo kuelekea Afrika Kusini katika club ya Super Sports kwa ajili ya kufanya majaribio ya wiki mbili katika club hiyo yenye makazi yake Pretoria na inatumia uwanja wa nyumbani wa Lucas Moripe.
Mbaga ameondoka leo akiwa na baraka zote kutoka kwa uongozi wa club yake ya Yanga SC, kama Gadiel Michael atajiunga na Super Sport itakuwa ni fursa nzuri kwake na kwa taifa kutokana na Ligi ya Afrika Kusini kuwa juu,hata hivyo atakuwa anaungana na mtanzania mwenzake Abdi Banda anayecheza Ligi ya nchi hiyo akiwa na Baroka FC.

Gadiel Michael
Club ya Super Sports ni club inayomilikiwa na kampuni ya vituo vya TV vya Super Sports nchini Afrika Kusini na ilianzishwa 1994, msimu wa 2017/2018 timu hiyo ilimaliza nafasi ya 7 katika msimamo wa Ligi Kuu nchini Afrika Kusini, msimu huu Super Sports ipo nafasi ya 5 ikiwa na point 39 tofauti ya point 4 dhidi ya Mamelod Sundowns wanaongoza Ligi .

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list