We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Friday, March 29, 2019

CCM Mkoa wa Dodoma yasikitishwa na hali ya ufaulu


Na,Enock Magali,Dodoma 

Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma kimesikitishwa na ufaulu hafifu unaosababisha mkoa kushika nafasi za mwisho kitaifa huku kikimtaka Afisa Elimu wa mkoa wa Dodoma ajitafakari na akiona ameshindwa kupandisha ufaulu aachie ngazi. 

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa huo Godwin Mkanwa wakati akichangia hali ya elimu katika mkoa wa Dodoma  katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa huo kilichofanyika jijini hapa. 

“Muungwana ni vitendo ,ukiona uungwana umekushinda jiengue mwenyewe,kwa hiyo Afisa Elimu jipime ,kama mambo yameshindikana ,chakula hakiivi ,nyanyua mikono, 
“Kasome ilani ya CCM ,kama huwezi kuitekeleza pisha,tunataka mabadiliko ya kifikra na kiutendaji.”alisema Mkanwa 

Aliongeza kuwa,yeye kama kiongozi aliyekabidhiwa dhamana ya  Elimu anatakiwa kuonyesha njia ya nini kifanyike ili mkoa uweze kuongeza ufaulu na kuondoka katika nafasi za mwishoni kitaifa hususani katika matokeo ya darasa la saba. 

Akichangia hoja Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kongwa White Zuber alisema aliwahimiza wajumbe wa kikao hicho kuimarisha vikao vya wadau katika kila wilaya kuzungumzia masuala ya elimu na kutatua changamoto za kielimu zinazowakabili. 

Alisema,suala la chakula cha  mchana linapaswa kupewa kipaumbele hata kwa shule za mijini kwa lengo la kuwafanya watoto kuvutiwa kukaa shuleni kusoma. 

”Suala la chakula liwe la mkoa mzima,watoto wale chakula ,sisi Kongwa tumeanza na ufaulu unaendelea vizuri ,jamii lazima ichangie .”alisema Zuber 

Naye Mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde alisema ,mimba bado ni tatizo  kwa watoto wa kike huku akisema mwaka huu pekee wanafunzi tisa wamepata katika shule ya Mvumi Misheni. 

Awali akiwasilisha taarifa ya maendeleo yua elimu mkoani humo,Afisa Elimu huyo alisema katika matokeo ya darasa la saba mwaka 2018 mkoa wa Dodoma umeshuka nafasi mbili na kushika nafasi ya 19  kutoka nafasi ya 17 mwaka 2017,hali iliyoamsha ari ya wajumbe.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list