We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, March 28, 2019

Cardi B afunguka jinsi alivyokuwa akitumia madawa, kuwalewesha wanaume pindi walipotaka kushiriki tendo la ngono

Cardi B alijitetea baada ya picha ya video iliyokua ikizunguka akionekana akisema kuwa aliwalewesha na kuwaibia wanaume waliokuwa wakitaka kushiriki ngono naye wakati alipokua akifanya kazi ya kunengua kabla ya kuwa maarufu.


attends the Billboard 2018 R&B Hip-Hop Power Players event at Legacy Records on September 27, 2018 in New York City.

Mwanamuziki huyo wa miondoko ya rap alikosolewa baada ya video hiyo ya Instagram iliyorekodiwa miaka mitatu iliyopita kusambaa tena mitandaoni.
”Sijawahi kusema kuwa mimi ni msafi sana au natoka ulimwengu ulio mzuri sana”.Alisema mwanadada huyo.
Awali video hiyo ilirekodiwa wakati ndio ameanza kazi yake na lilikua jibu kwa mtu aliyesema kuwa hana haki ya kuwa mwenye mafanikio kwa kuwa hafanyi kazi yoyote.
”Hakuna nilichokua napata.Hakuna,” alisema kwenye video hiyo, kabla ya kuweka wazi kuwa alikua akiwaalika wanaume kwenye hoteli kabla ya kuwanywesha na kuwaibia.



Akijibu shutuma hizo , aliandika kwenye ukurasa wa Instagram alieleza kuwa alikua akizungumza mambo ambayo yalikwishapita mazuri au mabaya ambayo yalinisaidia kuishi”.
Aliongeza:”Mimi ni sehemu ya utamaduni wa hiphop ambapo unaweza kueleza wapi umetoka , na hata mambo mabaya uuliyoyafanya kufika ulipo leo.” Mshindi wa tuzo za Grammy pia alieleza kuwa kuna wanamuziki ambao wanasifu mauaji, vurumai, dawa za kulevya na wizi”.
Aliandika: ”Sikuwahi kujisifu kwa vitu vilivyojitokeza kwenye video, sikuviweka kwenye muziki kwa sababu sijivunii na ninawajibika kutosifia.
Cardi B alimaliza kwa kueleza wanaume aliowazungumzia kwenye video yake ya zamani kuwa walikua wanaume aliokua na mahusiano nao na walikua wanajua wanachokifanya”.



Mapema juma hili, Hashtag ya #SurvivingCardiB ilikua imesambaa -ikifananishwa na Makala ya R Kelly, iliyoeleza miaka ya shutuma za ngono dhidi yake.
Baadhi ya watuamiaji wa mitandao ya kijamii wanamfananisha na mchekeshaji Bill Cosby, ambaye alihukumiwa kifungo mwaka 2018 baada ya kushutumiwa kuwalewesha wanawake kwa madawa na kuwadhalilisha.



Wengine wa mitandao ya kijamii walimtetea Cardi B kwa kuwa muwazi.






Male rappers on the come up :

I sold drugs. I pimped women. I robbed people. I did fraud & scams. I shot people. Anything to survive.

Twitter: @iamcardib: when guys offered me money for sex I would drug them and just take the money.

Twitter:


Mapema mwaka huu,Cardi B aliweka historia alipokua mwanamke wa kwanza akiwa muimbaji wa peke yake kupata tuzo ya Grammy kwa kuwa na albamu bora ya muziki wa kufokafoka yenye wimbo wake wa Invasion of Privacy.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list