We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Sunday, February 24, 2019

Ishu ya kutakiwa Azam Fc, Zahera afunguka


Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amewatoa wasiwasi Wanachama na Mashabiki wa timu hiyo kuwa hana mpango wa kuondoka Yanga


Tangu jana zilisambaa taarifa za Zahera kujiunga na Azam Fc, mtandao wa EATV ukiripoti kuwa kocha huyo atatangazwa kuwa kocha Mkuu wa Azam Fc wakati wowote

"Taarifa hizo hazina ukweli wowote, mimi nina mkataba na Yanga," amesema Zahera
"Hakuna mazungumzo yaliyofanyika kati yangu na Azam Fc. Siwafahamu viongozi wa Azam sijawahi kukutana nao mahali popote"

"Nawaambia Wana Yanga wapuuze taarifa hizo. Pia nawaambia wapuuze uzushi mwingi unaoenezwa juu yangu. Jambo lolote likitokea nitawataarifu mimi mwenyewe. Hata kama nikisafiri kwenda Congo nitawaambia"

Taarifa ya Zahera kutimkia Azam Fc imestua mashabiki wa Yanga hasa ikizingatiwa kocha huyo amekuwa chachu ya mafanikio ya kikosi cha Yanga msimu huu
Jana Azam Fc iliwafuta kazi kocha Hans van Pluijm na Msaidizi wake Juma Mwambusi na sasa inasaka warithi wa nafasi hizo

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list