We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, October 2, 2019

Kulthum Mansooor wa Takukuru amwandikia DPP barua ya kukiri makosa

Leo October 2, 2019 Aliyekuwa Mkurugenzi wa Mipango, Ufuatiliaji na Tathimini wa TAKUKURU, Kulthum Mansoor amemuandikia barua Mkurugenzi wa Mashtaka nchini(DPP) kwa ajili ya kukiri makosa yake .
Mansoor anakabiliwa na mashtaka manane ya kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha Sh.Bil 1.477.
Hayo yamebainika baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon kumueleza Hakimu Mfawidhi, Kelvin Mhina wa kuwa bado upelelezi wa kesi haujakamilika.
Baada ya kueleza hayo, Wakili wa Utetezi, Elia Mwingira amedai kuwa wameandika barua kwenda kwa DPP kwa ajili ya kuomba msamaha na kukiri makosa hivyo ni vyema kupata majibu kwa haraka ili mshtakiwa aweze kupata haki yake ya msingi.
“Tunaomba upande wa mashtaka kulifuatilia hili ili mteja wetu aweze kupata haki yake ya msingi,” alidai Mwingira.
Baada ya maelezo hayo Wakili Simon amedai kuwa suala hilo atalifuatilia kwa haraka zaidi.
Hakimu Mhina ameahirisha shauri hilo hadi Oktoba16, 2019 itakapokuja kwa ajili ya kutajwa.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list