Timu ya ZESCO United imewasili jijini Dar es salaam kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Yanga ambao utapigwa keshokutwa Jumamosi kwenye uwanja wa Taifa
Kocha Mkuu wa timu hiyo George Lwandamina, ameongoza msafara uliojumuisha wachezaji 19 akiwemo mkongwe Thabani Kamusoko
Akizungumza baada ya kutua JNIA, Lwandamina amesema amekuja nchini akifahamu anakabiliwa na mchezo mgumu mbele yake
Amesema licha ya kuondoka Yanga mwaka jana, timu hiyo imebadilika sana
"Yanga ni mpya.. ina kocha mpya, wachezaji wapya na viongozi wapya, mtu pekee ninayemfahamu ni kijana wangu Noel Mwandila..!," alisema
"Mchezo hautakuwa mwepesi lakini tumejiandaa kupambana kupata matokeo"

No comments:
Post a Comment