We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, September 12, 2019

Uwezekano wa maisha sayari nyingine wagundulika

Utafiti wa miaka ya karibuni katika anga za juu, umeonesha uwepo wa sayari nyingine nje ya mfumo wetu wa jua (Solar System), ambazo zinatajwa kuwa na uwezo wa kuruhusu uhai kwa wanyama na mimea lakini ugumu umebaki kuweza kuzifikia.
Unaambiwa kama chombo kitaweza kwenda spidi ya maili 35,000 kwa saa, itachukua miaka 40,000 kuweza kuikaribia sayari mojawapo, lakini inaelezwa uwepo wa ugumu wa kupita hata karibu ya Sayari hizo sababu zikitajwa ni uwepo wa mgandamizo mkubwa wa hewa pamoja na gesi nzito.
Utafiti mwingine wa hivi karibuni umegundua uwepo wa unyevu nyevu wa maji maeneo ya Sayari hizo, hivyo kuongeza uwezekano wa kuruhusu uhai kwa wanyama na mimea japo hiyo haitoi picha moja moja kwa sababu uwepo wa uhai hautegemei uwepo wa kitu kimoja bali vitu vingi.
Unyevu nyevu wa maji umegundulika katika sayari ya K2-18b ambayo kiumbo ni kubwa zaidi ya Sayari ya Dunia, lakini ina mfanano wa ukaribu wa hali ya hewa huku kukihisiwa kuwepo pia kwa vyanzo kama Bahari, Maziwa na Mito.
Mpaka sasa zimegundulika zaidi ya Sayari 2,000 ambazo zipo nje ya mfumo wetu wa Jua (Solar System), lakini imebaki kuwa ndoto kuzifikia sababu ya teknolojia iliyopo pamoja na ufinyu wa tafiti kuhusu maeneo hayo.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list