We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, September 26, 2019

Uhamiaji yawaonya wenye vyeti feki vya kuzaliwa

Idara ya uhamiaji nchini imetoa onyo kwa raia wasio Watanzania ambao wanaishi hapa nchini kwa kutumia vyeti feki vya kuzaliwa, na kuwa wakibainika watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwamo kukamatwa na kufikishwa mahakamani.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za idara hiyo mkoani Kagera, Kamishna wa Udhibiti na Usimamizi wa Mipaka nchini, Samwel Mahilane amewatahadharisha watu hao kuwa wasijione wako salama kutokana na kuishi hapa nchini kwa muda mrefu, lakini uhakiki ukifanyika watagundulika.
Kauli hiyo imekuja baada ya kukamatwa kwa raia mmoja wa Rwanda, Budugu Dudagali Sekalomba, aliyekuwa akitumia cheti cha kuzaliwa alichouziwa na Francis Izaya Makala, ambaye inadaiwa alikwishaondoka hapa nchini.
"Wasitumie vyeti vya watu wengine, kwa sababu sisi tukihakiki ndio tutatambua mhusika mwenyewe kwahiyo niwammbie tu kuwa wataingia hasara, watalia na tutawashtaki", amesema Samwel Mahilane.
Aidha kamishna huyo ametumia fursa hiyo kuwaonya raia wasio wa Tanzania ambao watajipenyeza kuingilia uchanguzi wa serikali za mitaa kuwa watakamatwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria. 

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list