Kocha Msaidizi wa Yanga Noel Mwandila amesema kikosi cha timu hiyo kiko tayari kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya ZESCO United ambao utapigwa kesho Jumamosi kwenye uwanja wa Taifa
Mwandila alimuwakilisha kocha Mwinyi Zahera kwenye Mkutano wa Waandishi wa habari ambao uliwahusisha makocha wa timu zote
"Tumefanya maandalizi ya kutosha, timu yetu iko tayari kwa ajili ya mchezo wa kesho," amesema
Mwandila pia amethibitisha kuwa Yanga itawakosa mshambuliaji David Molinga na beki Suleyman Mustafa ambao leseni zao bado hazijafika kutoka Shirikisho la soka barani Afrika (CAF)
Kwenye Mkutano huo, Mwandila alikutana 'uso kwa uso' na kocha George Lwandamina kocha wa ZESCO United ambaye ndiye aliyemleta klabu ya Yanga mwaka 2016 wakati akiwa kocha Mkuu

No comments:
Post a Comment