We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, September 11, 2019

Serikali yaingilia kati suala la Nyoka aliyezua gumzo Chato


Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori nchini Tanzania (Tawa) imemchukua nyoka mkubwa aina ya chatu aliyeonekana katika kijiji cha Kasala kata ya Makurugusi wilayani Chato mkoani Geita.

Kwa mujibu wa ofisa habari wa halmashauri ya wilaya ya Chato,  Richard Bagolele amesema nyoka huyo anapelekwa pori la akiba la Kigosi wilayani Kahama kuhifadhiwa.
Nyoka huyo anayeanza kuonekana siku saba zilizopita aligeuka kivutio kwa wananchi waliodai kuwa ni baraka, wengi kushinda porini wakimtazama huku wakiwa na mbuzi, maji na unga wakiamini endapo nyoka atakula watapata baraka ya mvua, kuongezeka kwa mavuno.
Akizungumza leo Jumatano Septemba 11, 2019 amesema Tawa iliwatafuta wataalam wa nyoka kutoka makumbusho ya Bujora waliofanikisha kumchukua noka huyo aliyekuwa katika kichuguu akiwa amelalia mayai 20.
Mmoja wa Wananchi wa kijiji hicho,  Philipo Maduhu amesema nyoka huyo ni baraka kwao na halmashauri haikupaswa kumuondoa.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list