We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, September 16, 2019

Mwanafunzi wa shule ya msingi akana kupewa mimba na mkuu wa shule

Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Kigoma imemuachia huru Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Nyantore wilayani Kigoma baada ya upande wa mashtaka kuomba kutoendelea na shauri hilo kufuatia shahidi wa pili mwanafunzi mwenye mimba kueleza mbele ya mahakama kuwa hamfahamu mtu aliyeshiriki naye mapenzi hadi kupata mimba.
Lakini pia shahidi huyo amekana kuwa na umri wa miaka 16 kama upande wa mashtaka ulivyoeleza awali kupitia upelelezi wa polisi.
Naye baba wa mwanafunzi huyo amesema kuwa binti yake ana umri wa miaka 19 na kwamba polisi walikuwa wakimshawishi aseme ana umri wa miaka 16 tofauti na anavyofahamu.
Kesi hiyo kwa mara ya kwanza ilisomwa Agosti 14, 2019 ambapo shahidi wa kwanza mama mzazi wa mwanafunzi huyo, Sakina Kazili (55) aliiambia mahakama Septemba 12 binti yake ana umri wa miaka 16 na kwamba alizaliwa februari 7, 2003.
Hakimu mfawidhi wa mahakama, Flora Mtarania amesema anakubali ombi la upande wa mashtaka kufuta shauri hilo na kwamba uamuzi huo hauzuii kumkamata tena mtuhumiwa huyo, Jason Rwekaza endapo atabainika kuwepo sababu za kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list