We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, September 3, 2019

Mmoja wa pacha waliotenganishwa afariki dunia

Mmoja wa pacha waliotenganishwa nchini Saudi Arabia na kurejea nchini Agosti 30, mwaka huu, Anisia Bernard, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Septemba 3.
Daktari aliyekuwa akiwahudumia watoto hao, Dk. Petronila Ngiloi amesema chanzo cha pacha huyo kupoteza maisha ni baada ya kutapika kwa muda mrefu na matatizo kwenye utumbo hali iliyosababisha kupoteza maji mengi na kushindwa kula chakula.
“Tangu walivyotoka safarini mmoja alionekana hakuwa na hali nzuri na tulivyotoka uwanja wa ndege tulikwenda moja kwa moja hospitali kumfanyia uchunguzi baada ya kuanza kutapika na kupandisha homa, hali hiyo iliyosababisha ashindwe hata kula lakini tukiwa kwenye ndege alikuwa anatapika.
“Hata hivyo vipimo ulioonesha kulikuwa na hitilafu kwenye utumbo ulikuwa umejikunja tulimfanyia upasuaji lakini hali iliendelea kuwa mbaya na baadaye kupoteza maisha akiwa ICU,” amesema Dk. Ngiloi.
Pacha hao Anisia na Melnes, walizaliwa January 29, mwaka jana wakiwa wameungana huko Misenyi mkoani Kagera na kupelekwa nchini Saudi Arabia kwa ajili ya kutenganishwa kazi iliyofanikiwa na kurudishwa nchini Agosti 31, mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list