We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Sunday, September 15, 2019

Manara amvaa Kindoki, mwenyewe ampa majibu haya

Msemaji wa Klabu ya Simba Haji Manara ameonekana akitupiana maneno na Mjumbe wa Kamati ya Hamasa wa Yanga, Jimmy Kindoki, ikiwa ni siku chache baada ya kumalizika kwa sare ya 1-1 katika mchezo wa kuwania makundi Ligi ya Mabingwa Afrika, dhidi ya Zesco United uliochezwa jana.

Maneno hayo yalianza kwa Haji Manara aliyepost video fupi katika mtandao wa Instagram ikimuonyesha Jimmy Kindoki huku ameandika kuwa
Nimesikitika sana mtu anayetambulika eti Mjumbe Kamati ya Hamasa ya Yanga kuwataka wafuasi wao wa-deal na washabiki wa Simba walioenda taifa jana, hii ni fedheha kwa mchezo wa mpira na aibu kwa klabu yake iliyompa 'dhamana' hewa, naomba tena na tena vitu hivi vya hovyo hovyo tuviache, laa sivyo soka tutaiharibu ladha yake” aamemandika Haji Manara
Akijibu madai hayo Jimmy Kindoki ameandika kuwaz “we mzee nakuheshimu ila unapoelekea sasa naona ni personal, hakuna sehemu niliyosema mashabiki wa Simba wapigwe wala hakuna video inaonesha nikimpiga mtu pale uwanjani, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Hamasa na si bondia"
Aidha Kindoki amedai kuwa Kazi yake ni kuhakikisha watu wanakuja uwanjani na hata wakienda washangilie mwanzo mwisho, asitake kuaminisha watu waliopigwa yeye ndiyo nimesababisha na hataki kugombana na watu wa Mashabikiwa Simba.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list