Haji Manara, Afisa Habari wa klabu ya Simba anafaamika zaidi kwa vituko na matukio mengi ya kufurahisha ambayo huyafanya
Baada ya Yanga kulazimishwa sare ya bao 1-1 na ZESCO United huku kiungo wa zamani wa timu hiyo Thabani Kamusoko akiifungia timu yake bao la kusawazisha kwenye dakika ya 94', Manara amejipachika jina la Kamusoko
"Naitwa Haji Thabani Scara Manara kamusoko," aliandika Manara kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram
ZESCO wameweza 'kuchomoa' kupoteza mchezo dhidi ya Yanga leo uwanja wa Taifa Kamusoko akifunga bao kwa shuti kali kwenye dakika za majeruhi

No comments:
Post a Comment