Mchezo wa kwanza wa ligi ya mabingwa kati ya Yanga dhidi ya ZESCO United uliopigwa uwanja wa Taifa umemalizika kwa sare ya bao 1-1
Mkongwe Thabani Kamusoko ndiye aliyeharibu sherehe ya Yanga akiifungia timu yake bao kwenye dakika za majeruhi
Patrick Sibomana alitangulia kuifungia Yanga bao la kuongoza kwa mkwaju wa penati kwenye dakika ya 25 baada ya Sadney Urikhob kuangushwa ndani ya eneo la hatari
Ni mchezo uliokuwa wazi kwa timu zote kuwa na vipindi vya kushambuliana kwa zamu
Yanga sasa ina kazi ya kusaka matokeo ugenini ili iweze kutinga makundi kama ilivyokuwa mchezo dhidi ya Township Rollers
Kikosi cha Yanga kimeonyesha kina uwezo wa kufanya vizuri kwenye mchezo huo wa pili

No comments:
Post a Comment