We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, September 12, 2019

Hakimu Dar Kortini kwa Tuhuma za Rushwa

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Kinondoni, jana Jumatano, Septemba 11, 2019, iliwafikisha mahakamani watuhumiwa watatu wa rushwa akiwemo Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo jijini Dar es Salaam, baada ya kukamilika kwa uchunguzi dhidi yao.

Takukuru imesema watuhumiwa hao ni Omary Mohammed Abdallah (40) aliyekuwa Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Magomeni jijini Dar, ambaye ni mkazi wa Kijitonyama kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa kiasi Tsh 703,000, Joseph Balongo (37) mfanyabiashara na mkazi wa Kibamba kwa kosa la kupokea rushwa ya Tsh 498,000 kinyume na sheria.

Imeelezwa kuwa, hakimu huyo alimtaka mtoa taarifa (jina limehifadhiwa na TAKUKURU) ampatie Tsh 1,000,000 ili amsaidie katika kesi ya mirathi iliyokuwa mbele yake. Baada ya Takukuru kufanya uchunguzi na kubaini kuwa ni kweli ilimtia nguvuni.

Aidha, Takukuru imemfikisha mahakamani Bw. Nelbert Malevo (33) mkazi wa Wazo, Dar es Salaam, ambaye ni Katibu wa Kamati ya Upimaji Viwanja katika Mtaa wa Nyakasangwe kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa. Inadaiwa kuwa aliomba Tsh milioni 2.5 na akapokea Tsh laki 5 ili ampe kiwanja mtoa taarifa (jina limehifadhiwa na Takukuru).

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list