Azam Fc imeanza vibaya mchezo wa kwanza wa kombe la Shirikisho raundi ya kwanza, baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Triangle United ya Zimbabwe
Licha ya kutawala mchezo huo kwa muda mwingi, safu ya ushambuliaji ya Azam Fc ilikosa umakini na kupoteza nafasi nyingi za kufunga
Bao pekee la Triangle United lilifungwa na Ralph Kawondera
Triangle United imemaliza rekodi ya Azam ya kutofungwa katika uwanja wa Chamazi
Mabingwa hao wa kombe la FA watalazimika kupata ushindi kwenye mchezo wa marudiano ugenini ili waweze kusonga mbele
Yanga na Azam Fc ndio timu pekee zilizobaki kwenye michuano ya CAF kutoka Tanzania baada ya Simba na KMC kutolewa katika hatua ya awali
Jana Yanga ililazimishwa sare ya bao 1-1 na Zesco United kwenye michuano ya ligi ya mabingwa
Nayo inahitaji matokeo ya ushindi au sare ya kuanzia mabao mawili ugenini ili iweze kusonga mbele hatua ya makundi

No comments:
Post a Comment