Jana kulikuwa na malalamiko mengi kutoka kwa mashabiki uwanja wa Taifa ambapo ilibainika kampuni ya Selcom ilikuwa ikiuza tiketi mara mbili kwa mashabiki waliokuwa wakiingia uwanjani kushuhudia mchezo kati ya Yanga dhidi ya Kariobang Sharks
Aidha kampuni hiyo pia ilikuwa ikiuza tiketi za Tamasha la Simba kwa mashabiki ambao walizitumia kushuhudia mchezo wa Yanga
Makamu Mwenyekiti wa Yanga Fredrick Mwakalebela amesema walithibitisha tiketi za mchezo wao dhidi ya Kariobang Sharks baadhi zilikuwa zikiuzwa mara mbili huku tiketi nyingine zikiwa ni kwa ajili ya mechi ya Simba lakini ziliuzwa kwa ajili ya mechi hiyo
Akizungumza na waandishi wa habari leo Makao Makuu ya klabu ya Yanga, Mwakalebela amesema baadhi ya watendaji wa Selcom waliokuwa wakiuza tiketi hizo wamekamatwa
Aidha uongozi wa Yanga umeandika barua Serikalini kuwajulisha jambo hilo ambalo wanaamini halina tija kwa maendeleo ya mpira wa miguu
Yanga inasubiri taarifa ya mapato yaliyopatikana kwenye mchezo huo ambayo bado haijatolewa na Selcom

No comments:
Post a Comment