We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, August 21, 2019

Waziri Jafo Atoa maagizo kwa Katibu Mkuu TAMISEMI

Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo, amemwagiza Katibu Mkuu wa ofisi hiyo, Joseph Nyamhanga, kuwarejesha mara moja katika kituo cha kazi cha Ipogoro, Manispaa ya Iringa watumishi saba ambao walihamishwa hivi karibuni.

Jafo alitoa agizo hilo jijini Dodoma jana wakati akifungua mkutano wa mwaka wa waganga wakuu wa mikoa na halmashauri.

Alisema kumekuwa na uonevu wa kuwahamisha vituo vya kazi baadhi ya watumishi jambo ambalo linawafanya wapoteze morali ya kazi.

Aidha, Jafo alimwagiza  Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Zainabu Chaula, kufuatilia kama mganga mkuu wa wilaya ameondolewa kazini kwa haki, kufanya makosa au kuonewa.

“Huyo mganga mkuu wa wilaya, alikuwa anafanya kazi yake kwa moyo, lakini hivi sasa ameondolewa kazini, sasa nataka ufuatilie je ameondolewa kwa makosa yake au nini kimetokea, fuatilia unipe majibu,”alisema.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list