We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, August 29, 2019

Wanaopiga muziki kwenye Magari, Kitchen party na Harusini kuanza kuwalipa wasanii (+video)

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe ametangaza kuwa kuanzia sasa, Watu wanaopiga nyimbo za wasanii wa muziki kwenye magari, kitchen party na harusini wataanza kuwalipa wasanii husika kwa kufuata utaratibu utakaowekwa.
Waziri Mwakyembe amesema huu sio wakati wa unyonyaji kama ilivyokuwa awali, Ambapo watu walikuwa wanakula jasho la wasanii bila aibu.
Waziri Mwakyembe ameyasema hayo jana kwenye mkutano na Wasanii wa muziki,  Waigizaji na wadau wa sanaa wa kujadili gawio la mirabaha na mapendekezo ya kuziunganisha Taasisi za BASATA, COSOTA na Bodi ya Filamu.
“Leo (Jana Agosti 28) ni mwisho kuburudika na kazi ya sanaa bila kuchangia chochote, kwenye kumbi zote iwe Harusi au kitchen party utachangia na hii si Dar es salaam bali ni nchi nzima maana huwezi kumlipa MC million 2 au 3 na usichangie hata 5% kwa muziki unaotamba nao kwenye sherehe hiyo,”amesema Waziri Mwakyembe.



No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list