We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Saturday, August 3, 2019

Mtangazaji wa DW afariki Dunia

Mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili (DW) Mohammed Dahman amefariki dunia siku ya Ijumaa (02.08.2019) Jijini Cologne, magharibi mwa Ujerumani.
Taarifa za kifo cha mtangazaji huyo mahiri zimetolewa na Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya DW, Andrea Schmidt
Mohammed Dahman alikuwa mwandishi wa habari mahiri katika nyanja zote, lakini alipendelea sana taarifa ya habari za ulimwengu na makala ya mbiu ya mnyonge.
Asilimia kubwa ya wasikilizaji walizipenda sana makala zake kuhusu masuala ya haki za binadamu na sauti yake ya huruma na alikuwa makini sana katika kuhakikisha taarifa zake pamoja na makala haziegemei upande mmoja.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkuu wa DW, Andrea Schmidt imesema kuwa, Dahman alikuwa akiugua kwa kipindi cha takribani miaka miwili na muda wote huo hakuweza kufanyakazi.
”Katika wakati huu mgumu wa majaribu, fikra na dua zetu tunazielekeza kwa mke wake, binti yake na familia yake visiwani Zanzibar na ughaibuni. Tunawapa pole na kutoa rambirambi zetu kwa majonzi makubwa, machozi yakitiririka machoni mwetu. Tunawaombea. Tulimpenda, lakini Mungu amempenda zaidi.”imeeleza taarifa hiyo

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list