We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, August 29, 2019

"Mpapaso tayari upo kwa Watanzania" - Masau Bwire

Afisa Habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire amesema kuwa kauli mbiu yao ya 'Kupapasa' tayari imeanza kujengeka kwa mashabiki wa soka baada ya kuwafunga Yanga hapo jana katika mchezo wa ligi.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Masau Bwire amesema kuwa kwa sasa Ruvu Shooting haina utani tena na ikitoa ahadi ya kupapasa, ni lazima iitekeleze.
"Ruvu Shooting wakikuambia wanakuja kukupapasa basi ujue wanakupapasa kweli na nikasema alama hiyo inaanza kujengeka kwa Yanga. Tayari alama ipo kwenye vichwa vya Watanzania kwamba hawa jamaa wanapapasa kweli", amesema Masau Bwire.
Katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania bara VPL hapo jana, Yanga ilikubali kichapo cha bao moja kutoka kwa Ruvu shooting na kuweka rekodi ya kupoteza kwa mara ya kwanza dhidi ya timu hiyo katika misimu mitatu ya karibuni.
Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera amekaririwa akisema kuwa chanzo cha kupoteza mchezo huo ni kutokana na uchovu wa wachezaji wake kwakuwa hawakuwa na muda wa kutosha wa kupumzika, huku akiitupia lawama Bodi ya Ligi kwa kukataa ombi lao la kusogeza mbele  mchezo huo.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list