Mwekezaji wa klabu ya Simba Bilionea Mohammed Dewji 'Mo' amesema ujenzi wa uwanja wa mazoezi wa Simba anaufanya kwa fedha zake mwenyewe na haupo kwenye mpango wa Bilioni 20 za uwekezaji
"Uwanja huu unajengwa kwa bajeti inayojitegemea tofauti na ile Tshbilioni 20 ambazo nilisema nitawekeza"
"Ninachotaka tuwe na miundombinu mizuri na tunajenga viwanja viwili ambapo kimoja ni cha nyasi bandia na kingine ni cha nyasi asilia,"
Aidha Mo amesema amefarijika kuona mashabiki na wanachama wengi wamekuwa tayari kushiriki kwenye mradi huo
"Tutaandaa utaratibu wa kuwashirikisha wadau wote kupitia michango yao ili itumike awamu ya pili ya ujenzi ambayo itahusisha ujenzi wa Hostel na maeneo muhimu ya huduma kwa ajili ya wachezaji"

No comments:
Post a Comment