We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, August 6, 2019

Mauaji Marekani: Trump akemea vitendo vya kibaguzi

Raisi wa Marekani Donald Trump amekemea chuki na imani kuwa mtu mweupe ana nguvu zaidi alipohutubia Umma baada ya tukio la mashambulizi yaliyogharimu maisha ya watu 31 katika miji ya Texas na Ohio.
Ametaka mabadiliko katika udhibiti wa silaha, na ametaka hukumu ya kifo iwakabili watu wanaotekeleza mauaji ya watu wengi, na kutazama tena sheria zinazohusu silaha.
''Ugonjwa wa akili na chuki hufyatua risasi, na si silaha,'' Trump alisema, akizungumza katika Ikulu ya Marekani siku ya Jumatatu.
Hakuonyesha kuunga mkono hatua za kudhibiti bunduki zilizopendekezwa katika Congress.
"Kwa sauti moja, taifa letu lazima likemee ubaguzi wa rangi, uhasama na mtazamo kuwa watu weupe ndio wenye nguvu," Bwana Trump alisema Jumatatu. "Mawazo haya mabaya lazima yashindwe. Chuki haina nafasi Amerika."
Maoni yake yalikuja muda mfupi kabla ya mtuhumiwa katika El Paso, Texas, kushtakiwa kwa mauaji . Polisi wa El Paso pia walithibitisha Jumatatu kuwa waathirika wengine wawili walikufa hospitalini, na idadi ya vifo vya Texas iliongezeka kufikia 22.

Trump amesema nini zaidi?

Rais alielezea sera kadhaa, ikiwemo pamoj ushirikiano zaidi kati ya wakala wa serikali na kampuni za vyombo vya habari vya kijamii, mabadiliko ya sheria za afya ya akili na kumaliza "utukufu" wa ghasia katika utamaduni wa Amerika.
Alitaka sheria kali zitakazoruhusu watekelezaji wa sheria kuchukua silaha kutoka kwa watu wanaoaminika kuwa tishio kwao wenyewe au kwa wengine.
Bwana Trump alisema mashirika ya serikali lazima yaweze kufanya kazi kwa pamoja na kubaini watu ambao wanaweza kufanya vitendo vya ukatili, kuzuia upatikanaji wao wa silaha za moto na pia alipendekeza kuwaweka kizuizini bila hiari kama njia ya kuwazuia washambuliaji.
Waombolezaji mjini DaytonHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Alisema pia alielekeza wizara ya sheria kupendekeza sheria kuhakikisha wale wanaotenda uhalifu wa chuki na mauaji ya watu wengi wanakabiliwa na adhabu ya kifo.
Rais alikosoa video za mitandaoni kwa kuchochea vurugu katika jamii.
"Ni rahisi sana leo kwa vijana wenye shida kujiingiza kwenye utamaduni unaosherehekea vurugu," alisema. "Lazima tuzuie au kupunguza hii na inapaswa kuanza mara moja."
Lakini hakuzungumzia ukosoaji kuhusu msimamo wake mkali dhidi ya uhamiaji haramu, ambao wapinzani wanasema umechangia kuongezeka kwa mashambulio yanayochochewa na ubaguzi.
Rais hapo awali alikuwa akiandika kwamba watunga sheria katika Congress wanapaswa kupitisha sheria za ukaguzi wa nyuma kwenye kifurushi na "mageuzi ya uhamiaji yanayohitajika sana".
Bwana Trump aliendelea kusema kuwa "yuko wazi na yuko tayari kujadili maoni yote ambayo yatafanya kazi" na akasema wanasiasa wa Republican na Democrats wanapaswa "kuungana pamoja kushughulikia hili.

Kilichotokea El Paso

Wachunguzi wanatazama kama shambulio lilichochewa na chuki, huku ikielezwa kuwa adhabu inaweza kuwa kifo.
Takriban watu 20 waliuawa huku wengine 26 wakijeruhiwa katika ufyatuliaji wa risasi katika duka la jumla mjini El Paso jimbo la Texas .
Gavana wa jimbo hilo Greg Abbot alitaja shambulio hilo kuwa mojawapo ya siku mbaya zaidi katika historia ya jimbo la Texas. Maafisa wa polisi wanachunguza iwapo shambulio hilo ambalo lilifanyika maili chache kutoka kwa mpaka wa Marekani na Mexico lilikuwa la uhalifu wa chuki.
Mtu mwenye umri wa miaka 21 kwa sasa anazuiliwa na maafisa wa polisi.
Waombolezaji mjini El PasoHaki miliki ya pichaAFP
kilichotokea Dayton
Kanda za video katika mitandao ya kijamii iliwaonyesha watu wakikimbia huku milio mingi ya risasi ikisikika katika barabara.
Inadaiwa kwamba shambulio hilo lilifanyika nje ya klabu ya burudani ya Red Peppers katika barabara ya tano ya E .
Klabu hiyo baadaye ilichapisha katika mtandao wa twitter ikisema wafanyakazi wake wako salama.
Polisi wanasema kuwa wote walioathirika walikuwa barabarani.
Polisi wanasema kwamba mshukiwa huyo alikuwa akiishi katika eneo la Allen , Dalla yapata kilomita 1,046 mashariki mwa El Paso. Ametajwa na vyombo vya habari vya Marekani kuwa Patrick Crusius.
Kanda za video za CCTV zilizodaiwa kuwa za mshambuliaji huyo ambazo zilionyeshwa katika vyombo vya habari vya Marekani zinaonyesha mtu aliyekuwa amevalia Tishati nyeusi pamoja na vilinda masikio.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list