We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, August 1, 2019

Manchester United waipa saa 120 Leicester City, liwake jua Inyeshe mvua Harry Maguire ni lazima atue Old Trafford, dau lake lamzidi Virgil van Dijk

Miamba ya soka nchini Uingereza Manchester United ipo tayari kuwapatia Leicester City pauni milioni 80 kwaajili ya kumnasa beki wao kisiki Harry Maguire.
Related image
Kwa mujibu wa talkSPORT timu hiyo ya Leicester imepewa siku tano kuanzia leo, hadi ifikapo Jumatatu ya wiki ijayo kuhakikisha inatoa majibu juu ya kukubaliana na ofa hiyo.
United inajaribu kutuma ofa ya pili baada ya ile ya kwanza ya dau la pauni milioni 70 kukataliwa na mabingwa hao wa zamani wa ligi kuu ya Uingereza.
Hata hivyo Leicester walikuwa wanahitaji kuhakikishiwa wanapata dau nono la zaidi ya pauni milioni 75 ambayo mabingwa wa klabu bingwa barani Ulaya Liverpool waliipatia Southampton kwa mchezaji wao Virgil van Dijk.
Kama mambo yatakwenda kama inavyotarajiwa Harry Maguire atasajiliwa kwa pauni milioni 80 ambalo litakuwa limezidi lile la beki bora kwa sasa duniani Virgil van Dijk alipotua Liverpool kwa pauni milioni 75 na kuweka rekodi.
Alhamisi ijayo dirisha la usajili linatarajiwa kufungwa, hivyo United inahaha kuhakikisha inamalizana na mchezaji huyo haraka iwezekanavyo.
Kwa upande wake Maguire amemuambia kocha wake ndani ya Leicester, Brendan Rodgers kuwa anahitaji kwenda kujunga na United

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list