We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, August 20, 2019

CPB Yampongeza Rais Magufuli Kwa Kuchaguliwa Kuwa Mwenyekiti Mpya Wa SADC

Salamu  za pongezi za kuchaguliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kuwa Mwenyekiti Mpya wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC zimeendelea kumiminika leo Agosti 20, 2019 ambapo Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) nayo imetoa salamu zake za pongezi.

"Bodi ya Wakurugenzi na Menejimenti ya Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) tunatoa pongezi nyingi kwako Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC kwenye kikao cha 39 cha Wakuu wa Nchi za SADC jijini Dar es Salaam 2019.

Tunakutakia Mheshimiwa Rais kazi njema na yenye ufanisi katika kutekeelza majukumu hayo mapya." Taarifa hiyo imesema.

Katika kikao cha kihistoria cha siku mbili kilichofanyika jijini Dar es Salaam Agosti 17 na 18, 2019, Wakuu hao wa Nchi walimchagua Dkt. Magufuli kuwa Mwenyekiti wa SADC kwa kipoindi cha mwaka mmoja ambapo aliyekuwa Mwenyekiti wa SADC Mhe. Dkt. Hage Gengob, ambaye ni Rais wa Namibia alimkabidhi uenyekiti huo.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list