We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, July 29, 2019

Vijana Mkoani Kagera Wahimizwa Kujitokeza Kugombea Nafasi Mbalimbali Za Uongozi

NA AVITUS BENEDICTO KYARUZI, KAGERA
Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi ccm taifa Kheri James amewataka vijana wenye sifa mkoani Kagera kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbali mbali kuanzia serikali za mitaa  ili waweze kuwatumikia wananchi katika maeneo yao.

Bwana Kheri James ametoa kauli hiyo july 27 mwaka huu katika uzinduzi wa Kagera ya kijani  uliofanyika katika uwanja wa Hamgembe uliopo katika manispaa ya Bukoba mkoani hapa.
Mwenyekiti huyo  amesema vijana ni nguzo kubwa katika ujenzi wa taifa hivyo wajitokeze ili kuwatumikia wananchi wao .
Ameongeza kuwa muda  wa kukaa vijiweni kwa vijana umeisha ambapo ametumia muda huo kuwahimiza viongozi waliopitia siasa kuwafundisha vijana wanaowania nafasi mbali mbali katika chama hicho kuwa na maadili mema ndani na nje ya chama hicho.
Ameongeza kuwa vijana watumie fulsa mbali mbali zitakazo wawezesha kupata mikopo kwani serikali ipo bega kwa bega na makundi muhimu likiwemo la vijana katika uzinduzi huo 

Bwana James amechangisha shilingi milioni kumi  zitakazotumika kuboresha  jengo la mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Elisha Marco Gaguti huku akipongeza juhudi za mkuu huyo wa mkoa katika maendeleo ya Kagera.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list