Viongozi wa nchi za Afrika wamekutana katika mkutano maalumu wa 12 wa nchi za Umoja wa Afrika unaofanyika nchini Niger.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya nchi hiyo, mkutano huo ulianza mjini Niamey chini ya ulinzi mkali.
Viongozi hao wa nchi za Afrika watajadiliana mambo mengi ikiwamo eneo la biashara huru barani Afrika (AfCFTA), matumizi ya pesa ya pamoja, masuala ya usalama, ugaidi na mambo mengineo.
Mwenyeji wa mkutano huo Rais wa Niger, Mahamadou Issoufou, alisema kupita kwa mkataba wa AfCFTA itakuwa ni faida kubwa kwa nchi zote za Afrika.
Umoja wa Afrika una jumla ya wakazi wapatao bilioni 1,2 na pato ghafi la dola trilioni 2,5.
Mkataba huo ulikubaliwa na nchi zote za Afrika isipokuwa Eritrea. Mkataba wa AfCFTA unaruhusu biashara za ndani ya bara kuwa na punguzo katika kodi ya forodha la asilimia 90.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya nchi hiyo, mkutano huo ulianza mjini Niamey chini ya ulinzi mkali.
Viongozi hao wa nchi za Afrika watajadiliana mambo mengi ikiwamo eneo la biashara huru barani Afrika (AfCFTA), matumizi ya pesa ya pamoja, masuala ya usalama, ugaidi na mambo mengineo.
Mwenyeji wa mkutano huo Rais wa Niger, Mahamadou Issoufou, alisema kupita kwa mkataba wa AfCFTA itakuwa ni faida kubwa kwa nchi zote za Afrika.
Umoja wa Afrika una jumla ya wakazi wapatao bilioni 1,2 na pato ghafi la dola trilioni 2,5.
Mkataba huo ulikubaliwa na nchi zote za Afrika isipokuwa Eritrea. Mkataba wa AfCFTA unaruhusu biashara za ndani ya bara kuwa na punguzo katika kodi ya forodha la asilimia 90.

No comments:
Post a Comment