We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, July 24, 2019

Kuiona Yanga, Kariobangi buku tano (5) tu


Uongozi wa klabu ya Yanga umetangaza viingilio katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Kariobangi katika Wiki ya Mwananchi kuwa ni Sh 5000 na VIP 100,000, mechi itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Agosti 4 mwaka huu.

Mchezo huo maalumu kwa ajili ya kutambulisha wachezaji wao unatarajiwa kuchezwa saa kumi jioni ambapo utatanguliwa na mechi kati ya Bongo Fleva na Bongo Movi na mavetenali wa Yanga na Pamba.
Akizungumza Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Hamasa wa klabu hiyo, Deo Muta alisema mchezo huo utakuwa katika viingilio vitatu ambapo kiingilio cha chini ni Sh 5,000 kwa mzunguko wa orange.
Muta alisema kwa upande wa VIP B kiingilio kitakuwa Sh 30000 wakati VIP A itakuwa ni Sh 100,000.
"Tunawaomba mashabiki wetu na wadau wa soka kujitokeza kwa wingi kuja kushuhudia usajili bora uliofanywa na klabu yetu ikiwa ni sambamba na burudani kutoka kwa wasanii na wakongwe wa ligi."
"Kutakuwa na wakongwe waliofanya kazi kubwa kipindi hicho Yanga ambao naamini kuwa watu hawawafahamu tutaweka majina kwenye jezi zao watakazovaa wakati wa kucheza ili kuondoa tabu kwa mashabiki kushindwa kutambua nani anamiliki mpira," alisema Muta.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list