Aliyekuwa beki wa Yanga Gadiel Michael ameuomba radhi uongozi wa timu hiyo kufuatia sintofahamu ya usajili wake
Aidha Gadiel amemuomba radhi wakala wake Jemedari Said ambaye ndiye aliyekuwa akimsimamia kabla ya kumzimia simu katika mazingira ya kutatanisha
"Wakati mwingine mtu unalazimika kufanya maamuzi yako peke yko kwa sababu anaewajibika na maisha yako mwisho wa siku ni mtu mwenyewe," amesema
"Mpira ndio kazi yangu ya kimaisha, maamuzi niliyoyafanya yalikuwa ni muhimu sasa kwa maslahi yangu na familia yangu
"Nimuombe radhi aliyekuwa meneja wangu Jemedari Saidi kazumari kutokana na sintofahamu iliuotokea kwa kutomshirikisha nikiamini asingekubali nihame mtaa.
"Nimelazimika kufanya maamuzi magumu kwa maslahi mapana yangu mwenyewe na familia yangu"
Kikubwa ni kwamba Mpira ni familia moja, bado tuko kwenye familia, HAKUNA CHUKI, MAISHA YAENDELEE
"Niwashukuru wanaYanga wote kwa ushirikiano walioniptia, nilikuwa na furaha sana kwao. Pia niwashukuru viongozi wa Yanga chini ya mzee Msolla. Mimi ni mwanadamu, kiumbe dhaifu, Maana aliekamilika ni mola wetu pekee"
"Nawaomba radhi sana"

No comments:
Post a Comment