We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Sunday, July 7, 2019

California yakumbwa na tetemeko kubwa kuwahi kutokea ndani ya miaka 20

CALFONIA-MAREKANI
TETEMEKO kubwa la ardhi kuwahi kutokea ndani ya kipindi cha miaka 20, limepiga kusini mwa mji wa California.
Mbali na California  baadhi ya maeneo ya Nevada nchini Marekani nayo yalikumbwa na tetemeko kama hilo.
Tetemeko hilo lilitokea juzi wakati Marekani ikiadhimisha siku yake ya uhuru na kusababisha majeruhi na uharibifu na kutokana na  matetemeko mengine madogo ya ardhi.
Wakati baadhi ya vyombo vya habari vikiripoti kuwa tetemeko hilo lilikua na  na ukubwa wa 7.1  katika kipimo cha Richter vingine viliripoti  ukubwa wa 6.4 ambalo lilipiga jangwa la Mojave, umbali wa kilomita 240 kaskazini mashariki mwa Los Angeles, karibu na mji wa Ridgecrest, California.
Mtaalamu wa miamba, Dk. Lucy Jones alisema tetemeko hilo linaweza kuendelea.
“Hili ni tetemeko ambalo linaweza kuendelea,” alisema katika mkutano wake na waandishi wa habari.
“Kila tetemeko linaweza kufanya tetemeko jingine,” alisema na kuongeza kuwa kulikuwa na uwezekano wa asilimia 10 wa tetemeko kama hilo au zaidi ya hilo  kutokea wiki ijayo.
Tetemeko hilo mbali na kuathiri Las Vegas na jimbo jirani la Nevada pia limeathiri maeneo ya mpakani na Mexico.
Gavana wa California, Gavin Newsom  alitoa msaada wake kwa watu alioathirika na tetemeko hilo, na kutoa wito kwa Rais kutangaza hali ya dharura pamoja na kutoa misaada.
Mkuu wa kikosi cha zimamoto, David Witt amethibitisha watu kadhaa kujeruhiwa na kwamba nyumba zilishika moto katika mji huo ulio na wakazi elfu 28.
Timu ya dharura ya uokoaji iliukabili moto mdogo, uvujaji wa gesi na ilikuwa ikishughulikia ripoti za barabara zilizopasuka kutokana na tetemeko hilo.
“Tumepata matatizo ya moto, gesi zimevuja, kuna majeruhi, watu hawana umeme, tunafanyia kazi yote kadiri inavyowezekana,”  Meya wa Ridgecrest, Peggy Breeden  aliliambia shirika la habari la  Reuters

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list