Aliyekuwa nahodha wa Yanga Ibrahim Ajib amewashukuru wadau wa Yanga kwa kumuunga mkono katika miaka miwili aliyoitumikia timu ya Wananchi
Ajib amesema amejifunza mengi Yanga na anaamini elimu hiyo itamsaidia kumjenga zaidi
"Hakika Ilikua miaka miwili bora sana kwangu, ndani na nje ya uwanja, Yanga ilikua sehemu ya familia yangu"
"Nitoe shukrani zangu za dhati kwa viongozi, benchi la ufundi, wachezaji na mashabiki wote, kwa kuniamini na kuniunga mkono katika kila jambo"
"Ni mengi nimejifunza na nina amini yatanisaidia kunijenga zaidi kama mchezaji. Asanteni sana"
"Hadi wakati mwingine tena, Wananchi..!"
Ajib amesajiliwa na Simba kwa mkataba wa miaka miwili

No comments:
Post a Comment