We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, June 20, 2019

Uwoya kufunga ndoa kwa mara ya tatu

Mlimbwende kutoka kiwanda cha 'Bongo Movie' Irene Uwoya anatarajia kufunga ndoa hivi karibuni lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida amesema hatohitaji mchango wowote kutoka kwa mtu yeyote zaidi ya ushirikiano.

Kwa mujibu wa chanzo cha karibu na Uwoya kimesema kuwa mwanadada huyo ni kweli ameanzisha kikundi cha 'Whatsapp' na kusema dhamira yake hiyo lakini kutoa kauli ya kusisitiza kwamba hahitaji mchango wowote bali ni ushirikiano tu katika jambo hilo.
"Ni kweli hilo group lipo na amesema kama ulivyosikia hahitaji mchango wowote bali ni ushirikiano tu kutoka kwa wanatasnia, kitu ambacho tumeona sio kibaya ni jambo jema maana ameridhia mwenyewe na sio kwamba tumeshindwa kumchangia", kimesema chanzo hicho. 
Muigizaji Irene Uwoya akifunga ndoa hiyo itakuwa ni ya tatu baada ya ile ya kwanza ambayo alifunga mwaka 2007 na kufanikiwa kupata mtoto mmoja ambaye ni Krish na aliyekuwa raia wa Rwanda na mchezaji wa soka marehemu Hamad Ndikumana na nyingine alifunga na msanii wa muziki wa bongo fleva Dogo Janja ambayo imedumu kwa muda mfupi.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list