We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, May 30, 2019

Juuko kuondoka Simba baada ya mkataba kumalizika

Beki wa Kimataifa wa Uganda Juuko Murshidi amemaliza mkataba na klabu ya Simba na yuko mbioni kujiunga na moja ya timu za ligi kuu Afrika Kusini
Juuko aliyeitumikia Simba kwa misimu mitano, aliondoka mapema kwenye kikosi cha timu hiyo kujiunga na kambi ya timu ya Taifa ya Uganda huko Arabuni
Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitte, Juuko amethibitisha kuwa hataendelea kuitumikia Simba msimu ujao
"Napenda kuwashukuru kwa kipindi chote kizuri tulichokuwa pamoja. Ilikuwa ni safari nzuri kwani tulishirikiana pamoja ingawa wakati mwingine inatubidi kila mmoja kuwa mbali na wengine," aliandika Juuko
Juuko alikuwa miongoni mwa wachezaji waliokuwa na mchango mkubwa kwenye kikosi cha Simba hasa katika michuano ya ligi ya mabingwa ambayo Simba iliondoshwa kwenye hatua ya robo fainali
Mwezi Disemba mwaka jana, Simba ilimuongezea mkataba wa miezi sita ambao unamalizika leo May 30

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list