We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, April 1, 2019

Tetesi za Usajili barani Ulaya Jumatatu hii, Bale, Wan-Bissaka, Mata, Siewert, Herrera, Tielemans na wengine sokoni

Mkufunzi wa Real Madrid Zinedine Zidane anasema kuwa hatma ya mshambuliaji wa Wales Gareth Bell ,29, ambaye amehusishwa na uhamisho wa kuelekea Man Unted mbali na kurudi Tottenham, utaamuliwa mwisho wa msimu huu.(Talksport)



Mkufunzi wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer anafikiria kuwasilisha dau la £35m ili kumnunua beki wa kulia wa Crystal Palace Aaron Wan-Bissaka, 21. (Mail)
Barcelona imewasiliana na babake Juan Mata na ajenti Juan Sr kuhusu uwezekano wa kiungo huyo wa Manchester United, 30 na Uhispania ambae kandarasi yake imekwisha kuhamia katika klabu hiyo..


Ole Gunnar Solskjaer

Hatma ya siku zijazo ya Jan Siewert kama mkufunzi wa Huddersfield haijulikani baada ya kushushwa daraja katika ligi ya Uingereza kutokana na kuvunjika kwa uhusiano wake na wachezaji wapya wa klabu hiyo. (times)
Manchester United inakataa kukubali mahitaji ya mshahara wa Ander Herrera wa £200,000 kwa wiki licha ya kandarasi ya kiungo huyo wa kati wa Uhispania mwenye umri wa miaka 29 kukamilika mwisho wa msimu huu mbali na kufuatiliwa na PSG . (Mirror)
Leicester inafikiria kuwasilisha dau la £40m ili kuimarisha mkopo wa kiungo wa kati wa Monaco na Ubelgiji Youri Tielemans, 21, kuwa uhamisho wa kudumu. (Mail)


Anders Herrera

Mkufunzi wa Everton Marco Silva anatumai klabu hiyo itachukua fursa nzuri iliopo kumsaini mchezaji wa Barcelona na Ureno aliyepo kwa mkopo Andre Gomes, 25, ambaye pia analengwa na Inter Milan, kwa mkataba wa kudumu. (Liverpool Echo)
Mkufunzi wa zamani wa klabu ya West Ham Harry Redknapp angependelea kumuona kiungo wakati wa Uingereza na nahodha Mark Noble, 31, kuifunza klabu hiyo siku moja baada ya kumaliza kucheza soka. (Star)


David Becham

David Beckham anasema kuwa mchezaji mwenza wa zamani Ole Gunnar Solskjaer anahitaji kuwa mkufunzi mpya wa Manchester United kutokana na kazi nzuri aliofanya wakati alipokuwa kaimu mkufunzi . (Manchester Evening News)
Arsenal inafikiria kumpatia mshambuliaji wake anayeuguza jeraha Danny Welbeck kandarasi mpya huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 akitarajiwa kuanza kufanya mazoezi kabla ya msimu huu kuisha. (Independent)


Danny Welbeck

Beki wa Everton na jamhuri ya Ireland Seamus Coleman, 30, anataka klabu hiyo kutumia fedha nyingi mwisho wa msimu huu iwapo itarudi kucheza katika kombe la Ulaya. (Independent)
Darren Moore amekiri alishangazwa alipotolewa nje kama mkufunzi wa West Brom . (Express and Star)
Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola anasema kuwa timu yake inahitaji kucheza mechi zake zote zilizosalia kama mashine iwapo inataka kushinda mataji manne msimu huu . (telegraph)


Pep Guardiola

Mkufunzi wa Chelsea Maurizio Sarri anasisitiza kuwa amezoea wito wa mashabiki wanaotaka afutwe kazi (Express)
Kiungo wa zamani wa Inter na Manchester United Juan Sebastian Veron, aliyeshiriki katika ufunguzi wa uwanja mpya wa Tottenham wikendi iliopita , anaamini Spurs itaweza kuvutia wachezaji wengi wa kiwango cha juu kutokana na nyumba yao mpya.. (Mirror)
Chanzo BBC.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list