We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, March 4, 2019

Waziri MPYA wa Mambo ya Nje Profesa Palamagamba Kabudi Atoa ONYO Kwa Wanaoichafua Tanzania

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi, amewataka watu wanaoisema vibaya Tanzania kukaa kimya kwa sasa.

Profesa Kabudi amesema hayo leo Jumatatu Februari 4, Ikulu jijini Dar es Salaam baada ya kuapishwa kuwa waziri wa wizara hiyo na Rais John Magufuli aliyemteua juzi baada ya kufanya mabadiliko madogo ya mawaziri.

“Jana haikuwa siku nzuri kwangu niliamshwa na watu wengine kuambiwa kwamba nimeteliuwa katika nafasi hii, lakini nashukuru kwa kunipa nafasi.

“Huu si wakati wa kuisema nchi yetu, kuibeza na kuipagaza… nchi yetu ilijengwa na mwasisi Mwalimu Julius Nyerere, yeyote Mtanzania mwenye tatizo na nchi hii atutendee jambo moja tu, akae kimya.

“Tuna jambo moja tu kubwa la kujenga mahusiano na wale wanaoitakia mema nchi yetu,” amesema Profesa Kabudi.

Pamoja na Profesa Kabudi, pia Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Augustine Mahiga aliapishwa na baadhi ya Makamishna wa Jeshi la Polisi.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list