We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, March 4, 2019

Tundu Lissu Afunguka Lowassa 'Kuinunua' CHADEMA

Tundu Lissu Afunguka Lowassa 'Kuinunua' CHADEMA
Mbunge wa Singida Mashariki na Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu amejitokeza na kumtakia heri Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa kufuatia uamuzi wake wa kurejea Chama Cha Mapinduzi.


Mbunge wa Singida Mashariki na Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu

Lowassa ametangaza kurejea CCM mapema Machi 1, 2019 ambapo alipokelewa na Mwenyekiti wa Chama hicho Dkt, John Pombe Magufuli katika ofisi ndogo za makao makuu ya chama hicho yaliyopo Lumumba Jijini Dar es salaam.

Lissu ameandika, "Edward Lowassa mwenyewe amesema amerudi nyumbani, maana yake ni kwamba alikuwa 'ugenini' tangu Julai 2015. hakuwahi kutuhonga wala kununua chama chetu kama tulivyotukanwa huko nyuma".

"Tulimkaribisha na kumpatia majukumu ya kutuongoza kwenye mapambano ya 2015. na alitekeleza majukumu hayo vizuri kwa kadri alivyoweza, na kadri tulivyomwezesha. matunda ya kazi yake, na ya kazi yetu yanajulikana", ameandika Lissu.

Lissu ameongeza kuwa, "na pengine sasa wataacha kumtishia kumnyang'anya mafao yake ya kisheria kama Waziri Mkuu mstaafu, badala ya kumlaani kwa kuondoka kwetu 'ugenini', mimi namtakia kila la kheri na mapumziko mema 'nyumbani' kwake sisi tutaendelea na safari yetu ya Canaan".

Wakati akipokelewa na uongozi mkuu wa CCM, Lowassa mwenyewe hakubainisha nini sababu ya kurejea CCM, bali aliishia kusema kuwa amerudi nyumbani.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list