We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, March 26, 2019

Ten afunguka maandalizi ya Yanga kuelekea mchezo dhidi ya Alliance Fc



Msemaji wa klabu ya Yanga Dismas Ten amesema kikosi cha timu hiyo kimepania kushinda mchezo wa robo fainali kombe la FA dhidi ya Alliance Fc utakaopigwa March 30 katika dimba la CCM Kirumba


Ten amesema Yanga imekuwa ikijifua katika uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini jijini Dar es salaam chini ya kocha Msaidizi Noel Mwandila ambaye ameachiwa program za mazoezi na kocha Mwinyi Zahera
Amesema baadhi ya wachezaji waliokuwa majeruhi tayari wameanza mazoezi kuelekea mchezo huo na anaamini mpaka siku ambayo kikosi kitaelekea Mwanza wachezaji wote watakuwa 'fit' kuikabili Alliance Fc

"Mchezo dhidi ya Alliance Fc tunauchukulia kwa umuhimu mkubwa kwani tukitwaa ubingwa wa FA tutajihakikishia nafasi ya kushiriki michuano ya Kimataifa msimu ujao," amesema Ten
"Hivyo hatuwezi tukaacha nafasi hiyo ipite kirahisi"

Juma Mahadhi na Raphael Daudi ni miongoni mwa wachezaji walioanza mazoezi ambao walikuwa nje kwa muda mrefu


TAFADHALI TUNAOMBA UTUPE NYOTA 5 KWA KU RATE APP YETU CHINI YA RADIO

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list